- ILI KUWEKEZA VIZURI MAISHA YAKO (1)
1. Tambua kuwa unapaswa kuwekeza Maisha - Tumepewa nafasi ya kuishi ili tuwekeze au tuitumie vizuri. Ni nafasi ambayo huja mara moja tu, ikiondoka hairudi tena.
- Muda wa kuishi si muda wa kuchezea, ni muda wa kuwekeza mahali panapostahili kwa ajili ya Mungu na kwa ajili ya watu.
- Maisha yetu yanapaswa kuleta faida na si hasara. Tunapaswa kufurahiwa na si kujutiwa.
- Maisha ni fursa, ni nafasi ya upendeleo, hatupaswi kuichukulia kiwepesi tu.
- Tumekuja duniani na hazina za kutosha ndani yetu, tunapaswa kuzitumia ili kuzalisha na kuleta manufaa duniani.
WEKEZA MAISHA