http://1.bp.blogspot.com/-eX2EwCM51-U/Vkn2JP2AZsI/AAAAAAACl0s/DxEglXXmumI/s640/Elias-Zacharia-akitoka-ndani-ya-shimo-futi-60-kutafuta-madini-ya-dhahabu-eneo-la-Nyakafandi-Nyanzari-wilayani-Ngara1.jpg
Siku ya tarehe 05/10/2015, wachimbaji wa dhahabu katika mgodi wa Nyangalata wilayani Kahama Shinyanga, walifukiwa na kifusi, mita zaidi ya mia chini ya udongo.
Ndugu na jamaa zao walishamaliza matanga, siku arobaini na moja baadae wakati wachimbaji wenzao wakiendelea na uchimbaji, walisikia ishara ya watu waliokuwa wakigongagonga kofia za plastiki na kuashiria kuomba msaada! Taarifa zilipelekwa sehemu husika, hatua zimechukuliwa, siku ya juzi watano wameokolewa wakiwa hai, mmoja alishakufa!
Huko udongoni waliishi kwa kula matope, matambala, na chochote walichoshika! Hadi wanaokolewa walikuwa hawaongei tena, walianza kuongea kesho yake.
Katika mazingira yale, hakukuwa na tumaini lolote, dakika yoyote walikuwa wanatarajia kukutana na Muumba wao!
Swali langu ni hili: Hivi kama wewe unajikuta kwenye mazingira kama hayo, ukiwa na akili timamu, unasubiri roho itoke ukiwa unaona! Je utakuwa na Amani unapojua kuwa muda si mrefu utakwenda kuvuna ulichopanda?
Hekima toka kwa mtumishi wa Mungu Alex Emmanuel Bubelwa
Katika mazingira yale, hakukuwa na tumaini lolote, dakika yoyote walikuwa wanatarajia kukutana na Muumba wao!
Swali langu ni hili: Hivi kama wewe unajikuta kwenye mazingira kama hayo, ukiwa na akili timamu, unasubiri roho itoke ukiwa unaona! Je utakuwa na Amani unapojua kuwa muda si mrefu utakwenda kuvuna ulichopanda?
Hekima toka kwa mtumishi wa Mungu Alex Emmanuel Bubelwa