Kanisa ABC Kahama


Tangu nimekuwa Mwalimu wa Neno la Mungu wa muda wote (Full time teaching minister) mwaka 2011, niligundua KANISA LINAUMWA UGONJWA WA UJINGA (KUTOJUA WANACHOKIAMINI, WANAYEMUAMINI, KUTOJUA HAKI ZAO NDANI YA KRISTO, MAMLAKA WALIYONAYO NA KIWANGO SAHIHI CHA MAISHA WANACHOPASWA KUISHI BAADA YA KUOKOKA KWA MUJIBU WA NENO LA MUNGU)… Hivyo Mungu aliponipa MAONO YA KUANZISHA MAKANISA YA ASSEMBLIES OF BELIEVERS (ABC), November 2016, msisitizo wangu mkubwa ni MAARIFA KWENYE MAENEO TAJWA HAPO JUU, NA USHIRIKA NA ROHO MTAKATIFU UNAOMFANYA KILA MSHIRIKA WETU KUWA ISHARA NA AJABU, AKITUMIWA NA MUNGU KUFANYA MAMBO YA KIUNGU KWA KANUNI RAHISI ZA UFALME WA MUNGU…. KWA KUJUA UMUHIMU WA SHULE (MAARIFA YA UFALME WA MUNGU), TUNA MADARASA KUANZIA JUMATATU HADI IJUMAA, KILA JIONI SAA 10-12:30… NA NDANI YA MIEZI MITATU YA KWANZA TUNA WASHIRIKA WANAFUNZI (WASIOKOSA HATA SIKU MOJA KATI YA HIZO WAPATAO 60), AMBAO WATAKUWA VIONGOZI MUHIMU KATIKA KUPANDA MAKANISA, NA KUUPELEKA UFALME WA MUNGU KILA AMBAPO MUNGU ATATUPA MLANGO ULIO WAZI.
Kama uko KAHAMA au una ndugu, Jamaa au rafiki aliyeko huku, tusaidie kumuunganisha nasi ili AKUE KATIKA SIRI ZA UFALME NA KUWA CHOMBO BORA CHA MAVUNO KATIKA SIKU HIZI ZA MWISHO.
..

.
Mchungaji na Mwalimu Dickson Cornel Kabigumila,
ABC Kahama, Nyahanga Kivulini.

Share on facebook
Share on twitter
Share on linkedin
Share on whatsapp
Share on telegram

USIOE KWA SABABU :2

  “Wenzako wote uliokua nao au kusoma nao wanaoa. Ndoa si ALISEREMA ARIJA AU MWENGE TUNAUKIMBIZA. Ndoa ni taasisi ambayo Mungu amemuwekea kila mmoja wetu

Read More »

HEKIMA ZA NDOA 5

“Ni mwanandoa mpumbavu pekee anayesubiri aombwe msamaha ili asamehe; Maana waweza kukuta kile unachoona kama kosa, mwenzako anaweza asikione hivyo, kwa kutosamehe ufa huo unaweza

Read More »