Shedraka, Meshaki na Abednego walijua siri hii ya ajabu. Walimjua Mungu wao. Walijua kuwa Mungu wao ni hai siku zote. Walijua anafanya kazi muda wote. Walijua yote yanawezekana kwake. Walijua yasiyowezekana kwao kama wanadamu, kwa Mungu wao, Jehova yanawezekana…WALIMWAMINI.
Hata ilipotokea JARIBU KUBWA KWAO LILILOGHARIMU MAISHA YAO…Bado walikuwa na Ujasiri wa kumwambia Mfalme Nebukadreza, “Mungu wetu tunayemwabudu aweza kutuokoa, lakini hata asipotuokoa na ijulikane ya kuwa hatukuisujudia sanamu yako” (Danieli sura ya 3).
Walikuwa na kiwango cha juu cha uelewa, walijua kuwa Mungu kutojibu Ombi lako sawa na ulivyomwomba haibadilishi Yeye kuendelea kuwa Mungu…Mtumishi wa Mungu Mwalimu Christopher Mwakasege amewahi kusema, “MUNGU ANABAKI KUWA MUNGU HATA KAMA HAJAJIBU OMBI LAKO KAMA ULIVYOMWOMBA”
Mungu asipofanya kile ulichomwomba, hasa pale unapokuwa umekiomba sawa na mapenzi yake [sawa na Neno lake] anakuwa na sababu…Pengine ameona kuna shida itatokea endapo ukipata kitu hicho na pengine utapoteza uhusiano wako na Yeye. Na kumbuka uhusiano wako na Mungu ni wa muhimu sana kuliko chochote mbele za Mungu…Pengine anataka kukupa kitu bora zaidi kuliko hicho ukitakacho sasa…Pengine anakuandaa kwa hatua fulani bora katika maisha yako..!
JIZOEZE KUMWAMINI MUNGU KATIKA HALI ZOTE, NJEMA NA MBAYA, NGUMU NA NYEPESI, KWENYE SHIDA NA RAHA…Haya ndiyo mapenzi yake kwako!
HII NAYO YA MUHIMU SANA KWA YULE UNAYEJIANDAA KUWA MME/MKE WAKE!
Luka 1:5 inasema kitu kuhusu Kuhani Zekaria, na Mke wake Elisabeth…na kuna mambo kadhaa ya kujifunza; 1.Zekaria alikuwa kuhani, lakini Elizabeth alikuwa wa Kabila la