Usipoteze Muda Kuyaweka Maneno Ya Wanadamu

 
Usipoteze Muda Kuyaweka Maneno Ya Wanadamu Kwenye Akili Yako… Wao Wakikwambia Hauwezi Kufanikiwa Au Kusogea Kwenye Maisha, Huo Ni Mtazamo Wao Na Si Wa Mungu… Hata Hivyo Mwanadamu Anajua Nini Kuhusu Yajayo? Yeye Anajua Yale Tu Anayoyaona Na Kuyasikia Ndani Ya Sekunde Aliyopo… Mwanadamu Anaweza Kukudharau Au Kukushusha Kwa Sababu Hali Yako Ya Uchumi Haiko Vizuri Leo, Lakini Hajui Kesho Unaweza Kukutana Na Vijisenti Vinazurura Ukavifuma… Wanadamu Wanafanya Makosa Makubwa Kwa Kukupangia Daraja Na Mipaka Ya Maisha Yako, Hawajui Kuwa Mungu Amekuumba Kwa Kusudi Na Mpango Maalumu… Hawajui Kuwa “You Are Loaded With Possibilities, Potentials, Talents, Gifts, Wonders etc” Wanafanya Kosa Kubwa La Kupima Kiasi Cha Mvua Kwa Kutazama Kiwango Cha Mawingu Yaliyoko Angani… Kamuulizeni Eliya na Ahabu, “WINGU KAMA NGUMI YA MTU” Lilimwaga Mvua Si Kawaida… Una Kila Kitu Ambacho Ni Rasilimali Ya Mungu Kuonesha Maajabu Yake Kupitia Wewe… Mimi Hakuna Wa Kuniambia Lolote Kuhusu Maisha Yangu, Hata Malaika Hawawezi Kuniambia Kina Cha Maisha Yangu… Najua Nimebeba Sura Na Mfano Wa Mungu, Naweza Kuumba DUNIA YANGU… Hapo Vipi? Bado Unajidharau Na Kujishusha? Unaweza Kufanya Chochote, Kila Kitu Utakacho Kupitia Kristo Akutiaye Nguvu!

Share on facebook
Share on twitter
Share on linkedin
Share on whatsapp
Share on telegram

usioe kwa sababu

“Usioe kwa sababu unawaka tamaa, hivyo unaoa ili usiendelee kutenda dhambi nje. Dawa ya tamaa si kuoa. Dawa ya tamaa ni kukubali kuwa tamaa inakutesa,

Read More »

USIOE KWA SABABU :2

  “Wenzako wote uliokua nao au kusoma nao wanaoa. Ndoa si ALISEREMA ARIJA AU MWENGE TUNAUKIMBIZA. Ndoa ni taasisi ambayo Mungu amemuwekea kila mmoja wetu

Read More »