Wanadamu Wana Maumivu, Vilio Na Matatizo Mengi, Wengi Wanayaonesha Na Kuyakiri Waziwazi Lakini Wachache Wanabaki Nayo Moyoni; Aidha Kwa Vile Wana Imani Kwamba Mungu Ataingilia Kati Na Kuwasaidia Ama Hawapendi Kuwapa Faida Watu Wengine!
LAKINI
Unapomshauri Mtu Au Kumtia Moyo Au Kumpa Faraja, Hakikisha Kwamba Hiyo Faraja Ni Ya KWELI… Kama Haina Ukweli, Hata Akifurahi Kwa Muda, Na Kucheka Kwa Kitambo, Siku Akijua UKWELI HALISI Lazima Atajuta, Ataumia Na Wewe Uliyempa Faraja Ya Uongo UTAKUWA ADUI YAKE NAMBA MOJA!
Iseme Kweli Hata Kama INAUMA Au Haipokelewi, Lakini Mhusika Akija Kujua Kwamba Ulichosema Kilikuwa KWELI HALISI, Atatambua Kwamba Ulikuwa MTU MWEMA Na Hata Asiporudi Kukushukuru Lakini Moyoni Mwake Atajua Kwamba ULIMTAKIA MEMA!!
“INUNUE KWELI WALA USIIUZE…”
“MUNGU ANAPENDEZWA NA KWELI ILIYOKO MOYONI”
“NA HIYO KWELI ITATUWEKA HURU, NASI TUTAKUWA HURU KWELI KWELI”
Salamu Toka Mwanza,
Mwl D.C.K
dicoka@rocketmail.com