Neno La Mungu

bible
neno la mungu

Kama NENO LA MUNGU halitendi kazi kwako itakuwa ni kwa sababu mojawapo kati ya hizi;
1.Hauna uhusiano na ushirika wa dhati na Mungu ila unataka kulitumia NENO kama mganga wa kienyeji…”Katika mambo yote, Mungu hutenda kazi na wale WAMPENDAO, AKIWAPA MEMA” (Rumi 8:28-29)
2.Umeyapa MASHAKA nafasi…”Mwenye mashaka/ nia mbili ni kama mawimbi upeperushwa huku na huko na mtu wa aina hii asitarajie k

itu toka kwa Mungu” (Yakobo 1:5-7)
3.Maisha yako si MASAFI…uko nusu nusu, kwa Mungu nusu, dunia nusu…Maisha yako yanapungukiwa na vitu muhimu kama vile MAISHA YA HAKI, UAMINIFU, UPENDO, DHAMIRI NJEMA MBELE ZA MUNGU (Isaya 59:1-2)
4.Umekosea matumizi ya NENO husika…haujafanya sawa na MAELEKEZO YA NENO (Kumbukumbu 28:1)
5.Una haraka, hautaki kuusubiri MUDA WA MUNGU…”God’s time is the best time” Prophet TB JOSHUA
“Kila jambo na muda wake…na majira kwa kila kusudi chini ya mbingu” (Mhubiri 3:1)
“…Yeye AAMINIYE[mtu wa IMANI] hatafanya haraka” (Isaya 28:16)
6.Kile unachotaka NENO likufanyie unakitaka kwa ajili ya TAMAA ZAKO MWENYEWE na kwa UTUKUFU WAKO MWENYEWE…”Lolote mfanyalo kwa neno au kwa tendo fanyeni kwa ajili ya utukufu wa Mungu”
Share on facebook
Share on twitter
Share on linkedin
Share on whatsapp
Share on telegram

usioe kwa sababu

“Usioe kwa sababu unawaka tamaa, hivyo unaoa ili usiendelee kutenda dhambi nje. Dawa ya tamaa si kuoa. Dawa ya tamaa ni kukubali kuwa tamaa inakutesa,

Read More »

KWA WAOAJI TU

“Ukimuona Mwanamke Ambaye AMEKAMILIKA TAYARI [Product] Ujue Kuna Mwanaume Mwingine Ambaye AMEINGIA GHARAMA Kumfanya AHAME TOKA KWENYE MALIGHAFI [Raw Material] Mpaka Kuwa Vile Alivyo… UKIONA

Read More »

HEKIMA ZA NDOA 5

“Ni mwanandoa mpumbavu pekee anayesubiri aombwe msamaha ili asamehe; Maana waweza kukuta kile unachoona kama kosa, mwenzako anaweza asikione hivyo, kwa kutosamehe ufa huo unaweza

Read More »