Elewa na kutambua haki yako

image
Moja kati ya mambo yanayochangia SWALA LA KURITHI LAANA toka kwa waliotangulia ni KUTOJUA KUWA WOKOVU UMEFANYA KWAKE YAFUATAYO…  Wokovu Umeshughulika na maeneo yote ya mtu; ROHO, NAFSI NA MWILI… Wakristo wengi sana (karibu wote) wanadhani WOKOVU umeshughulikia ROHO ZAO TU na umeacha NAFSI NA MIILI YAO ikiwa vilevile. Wanaupima na kuupokea Wokovu kwa HISIA… Wanajitazama, Wanajiona NDANI YA ROHO ZAO WAMEPATA UHAI, WANAICHUKIA DHAMBI, NA HAWANA TENA KIU YA DHAMBI mara baada ya MAOMBI YA IMANI KUMPOKEA YESU kupitia SALA YA TOBA… Lakini wanaendelea KUWA CHINI YA LAANA kwenye NAFSI (Eneo linaloshughulika na maswala yote ya AKILI, UFAHAMU, FIKRA, MAWAZO, MAAMUZI NA MACHAGUO) na kwakuwa wanaishi kwenye MIILI, LAANA ZINAONEKANA KWENYE MAISHA YAO kwa KUTOFANIKIWA KWENYE MASWALA NA MAENEO MBALIMBALI YA MAISHA, KUKWAMA, KUTOVUKA VIWANGO FULANI VYA MAISHA, KUKUMBWA NA MATUKIO MABAYA YALIYOWAHI KUWAKUTA WAZAZI, NDUGU WALIOWATANGULIA, KUKOSA AMANI NA FURAHA YA MAISHA, KUYACHUKIA MAISHA NA HATA KUCHUKUA MAAMUZI MABAYA IKIWEMO HATA KUJIUA, nk! UKWELI NI KWAMBA: Shetani anatumia NAFASI ALIYOPEWA na hawa WAKRISTO kwenye NAFSI NA MIILI YAO kwa kutojua (kukosa maarifa) kwamba WOKOVU NI UUMBAJI WA MTU KUFANYWA KIUMBE KIPYA KABISA AMBACHO HAKINA UHUSIANO NA MAMBO YA ZAMANI, ZIKIWEMO LAANA ALIZOKUWA NAZO KABLA YA WOKOVU (2 Kor 5:17)… Kiumbe huyu anapewa NAFSI MPYA; NIA/ AKILI YA KRISTO (1 Kor 2:16) inayomfanya awe na kiu ya KUFANYA MAPENZI YA MUNGU NA KUMPENDEZA MUNGU kama alivyokuwa Kristo Yesu… na mwisho kiumbe huyu aliyeokoka MWILI WAKE UMEUMBWA UPYA, Si ule uliokuwa ukikandamizwa na MAPEPO, NGUVU ZA GIZA, MIZIMU, UCHAWI, MAGONJWA nk, MWILI WA ALIYEOKOKA ni HEKALU LA MUNGU NA ROHO MTAKATIFU ANAKAA NDANI YAKE (1 Kor 3:16-17) na tangu hapo MUNGU ANACHUKUA UDHIBITI… Ila HAIFANYI KAZI Mpaka MWAMINI AJUE HILI, LIWE MFUMO WAKE WA MAISHA, UKIRI WAKE MBELE YA WATU NA SHETANI! Pia ni muhimu MKRISTO AELEWE NA KUTAMBUA HAKI, UHALALI,NA NAFASI YAKE MBELE ZA MUNGU kupitia AGANO JIPYA!

Share on facebook
Share on twitter
Share on linkedin
Share on whatsapp
Share on telegram

NDOA

Haikuanzishwa Na WANADAMU Bali MUNGU Ndiye Aliyeanzisha TAASISI HII… Imeanzishwa Na MUNGU Ambaye Ni Roho, Uwe Na Uhakika Haiwezi Kuendeshwa Kwa Kutegemea AKILI, HEKIMA NA

Read More »

USIOE KWA SABABU :2

  “Wenzako wote uliokua nao au kusoma nao wanaoa. Ndoa si ALISEREMA ARIJA AU MWENGE TUNAUKIMBIZA. Ndoa ni taasisi ambayo Mungu amemuwekea kila mmoja wetu

Read More »
Mafundisho
yesunibwana

SIFA ZA MME BORA

  1. Yeye mwenyewe AMEMPOKEA YESU, NA KUJITIA CHINI YA MAMLAKA YAKE KAMA BWANA NA MWOKOZI WAKE KIBINAFSI (Yohana 1:12-13, Yohana 3:16-18). -Atambue thamani ya

Read More »