KWA WOTE AMBAO MLIKUWA KWENYE MAHUSIANO HALAFU GHAFLA YULE ULIYEMPENDA AKAKUACHA BILA SABABU YA MAANA>>>Usimlilie, wala usiuumize moyo wako kwa ajili yake. Usijipe PRESHA bure kwa ajili yake. Huyo aliyekuacha hakuwa mtu sahihi. Mungu amekusaidia kumdhihirisha mapema kwamba alikuwa MBWA MWITU kwenye NGOZI YA KONDOO. Mshukuru sana Mungu, amekuondolea KICHOMI. Hebu fikiri, vp kama angeendelea kuficha makucha yake, ukaingia naye kwenye ndoa halafu ndo akakugeuka na kudai/kukupa talaka? Ingekuwa FEDHEHA kubwa. After all, wako wanawake/ wanaume wacha Mungu kibao ambao kila siku wanakata rufaa kwa Mungu ili wawe na wewe na wako serious, wamemaanisha kuutunza MOYO WAKO. Using’ang’anie VIMEO wakati ORIGINAL wapo! Anza kumpa Mungu utukufu maana anakupenda na amekuepusha na hilo JANGA KUBWA NA ZITO. Huyo mkaka/ mdada alitoka kwako lakini hakuwa wa kwako, Maana kama angalikuwa wa kwako angalikaa pamoja nawe.Lakini ameondoka ili afunuliwe kwamba si wote walio wa kwako ( 1 Yohana 2:19). ** Mwalimu anayapa maisha yako thamani anayoiona Mungu ndani yako**
Mafundisho
KWA WAOLEWAJI TU
“Kati Ya Mambo Unayopaswa Kuyachunguza Kuhusu Mtu Anayetarajia Kukuoa NI UAMINIFU NA UADILIFU Kwenye MALI NA PESA YA UMMA, KAMPUNI Au WATU WENGINE… Ukiona Huyu