“Njia ya tatu ya kufanya ili ULIVYONAVYO NDANI vitoke na vidhihirike NJE KWENYE DUNIA YAKO ni KUITUMIA IMANI KATIKA NENO LA MUNGU. Imani ni HAKIKA YA MAMBO YATARAJIWAYO. Imani haibahatishi, imani ni hakika! Imani ina uwezo wa KUYAZAA YASIYOKUWEPO UNAYOYATARAJIA. Imani huzaliwa kwa kusikiliza juu ya ahadi na kweli za Neno la Mungu zinazokujulisha kuwa MUNGU ANA VITU VIKUBWA VYA KUFANYA KUPITIA MAISHA YAKO (Vikiwemo hivyo unavyoona ndani yako). Pia IMANI INA NGUVU BINAFSI YA KUSUKUMA VITU VITOKEE (Imani huamisha milima, imani hufunga hata makanwa ya simba, imani huzaa miujiza, imani hushinda ulimwengu na kila kizuizi). Ukiwa na imani hata chembe ya haradali UTAZAA BARAKA NA IDEAS ZOTE ULIZOBEBA”
(Ebr. 11:1, Marko 9:23, Marko 11:23-24, Wagalatia 3:14, 1Yohana 5:1-4).
KILA MWANANDOA MTARAJIWA NA MWANANDOA TAYARI.
Jikumbushe haya kuhusu ndoa: 1. Ndoa ni agano la milele mpaka kifo (ajiandae kwa hilo kiakili, kiufahamu, kihisia na kiroho)! Ukikurupuka kama fashion au kufikiri