Kwako wewe usiyeamini

USHUHUDA…
BWANA Yesu asifiwe, leo ninao ushuhuda kwako, wewe usiyeamini ya kuwa Yesu wa Nazareth na Neno la Mungu ni hai hata sasa!
JUMANNE YA WIKI HII(14/08/2012), Yesu wa Nazareth amemponya kijana mmoja Ugonjwa wa Vidonda vya Tumbo sugu (Chronic Ulcers) ambao amekuwa nao kwa zaidi ya Miaka 7.
Kijana huyu nimekutana naye kwenye Ibada zinazoendelea kila jioni pale Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT)

kwa ajili ya Wanafunzi wa ACCESS COURSE…
Tatizo lake lilikuwa kubwa kiasi kwamba, hata kama angekunywa hata chai ilimbidi akimaliza tu ameze pia MAGNESIUM ili kutuliza maumivu na kuondoa gesi tumboni.
Kwahiyo kwa siku walau alimeza Magnesium mara tu hivi!
Kisha akaja pale Ibadani, akalisikia Neno la Mungu, Imani ikaja ndani yake, Nikaweka mikono juu yake halafu YESU KRISTO ALIYE HAI AKAMPONYA!
Kwa miaka zaidi ya 7 alikuwa hawezi kula maharage, pilipili na vyakula kadha wa kadha. Ila sasa anakula kila kitu, na hatumii tena Magnesium wala dawa yoyote…
UAMINI AU USIAMINI, HAITABADILISHA UKWELI YA KUWA YESU YU HAI NA ANATENDA KAZI SASA!
Mimi ni shahidi wa Nguvu na Utendaji wake, nadhibitisha ya kuwa Yesu wa Nazareth yu hai jana, leo na hata milele (Waebrania 13:8)!
Share on facebook
Share on twitter
Share on linkedin
Share on whatsapp
Share on telegram
Mafundisho
yesunibwana

KWA WAOLEWAJI TU

“Kati Ya Mambo Unayopaswa Kuyachunguza Kuhusu Mtu Anayetarajia Kukuoa NI UAMINIFU NA UADILIFU Kwenye MALI NA PESA YA UMMA, KAMPUNI Au WATU WENGINE… Ukiona Huyu

Read More »