THE POINT OF CHANGE

Point of Change
(C) @johngibbons -Unsplash

Sehemu ipi kwa mwanadamu ambayo ikihusishwa tu inaleta mabadiliko kwenye Maisha yake jumla ; mabadiliko kwenye tabia , ndoa, uchumi , kutoka dhambini
Kwa utafiki wangu ;
nilifikiri mchungaji akinyosha
mkono akasema ;

Fireeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee Fireeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee
Kwenye akili, kwenye nywele, kwenye Simu , kwenye nguo, kwenye ndoa yako
Na watu wakaanguka chini wote ; nilifikiri wakiinuka kwasababu ya fire tabia zao zitabadilika , lakini ndio wanaendelea vizuri
Nilifikiri Mtu wa Mungu akisema
Touch Touch Touch
Na watu wakaanguka ; nilifikiri watabadilika tabia, lakini hoo mambo yanabaki pale pale

KINACHOLETA MABADILIKO
kwenye Maisha ya mkristo aliyeokoka
ni maamuzi : maamuzi ya kulitii neno la Mungu bila shuruti ndicho kinacholeta mabadiliko
Unaweza kumuita mshirika ukamwambia simama pale , ukasema In the mighty Name of Jesus Christ touch , na akaanguka , na pepo wakatoka lakini kama hajaamua kubadilika ( nothing will happen )
Jaribu kufikiri

#Mwanzo 4:6-7
[6]BWANA akamwambia Kaini, Kwa nini una ghadhabu? Na kwa nini uso wako umekunjamana?
[7]Kama ukitenda vyema, hutapata kibali? Usipotenda vyema dhambi iko, inakuotea mlangoni, nayo inakutamani wewe, walakini yapasa uishinde.
Mwanadamu wa Kwanza hakushauriwa na baba yake, hakushauriwa na mchungaji , Alishauriwa na Mungu moja kwa moja ( Jaribu kufikiri ) , Ni Mungu ndiye aliyemshauri
Tuangalie Mungu anamwambia Kaini
Usipotenda vyema dhambi iko, inakuotea mlangoni, nayo inakutamani wewe, walakini yapasa uishinde.
( Mungu anamshauri kaini anamwambia
Hiyo dhambi kuishinda kuko NDANI uwezo wako )
Mimi nilifikiri kaini ataogopa na kuifanyia kazi sauti ya Mungu kwa kutetemeka LAKINI jamaa aliendelea mbele na kufikia
Lengo lake la kuua ( just imagine )

HAYA TUONGEE NAWATAALAMU WA LEO
Ukikaa kanisani unasikia maonyo ya Roho Mtakatifu juu ya hiyo tabia uliyonayo ambayo haimpendezi Mungu ( unachukua hatua gani ? ) Ukibisha , chunguza Kwanza moyo wako
Utagundua ile hali ya Kaini iko sana sana, watu wengi wanamsikia Mungu lakini wengi bado wanaendelea na kufuata uovu ( Hii ni hatari sana – you kill your life )
NITARUDIA TENA ! KITU GANI KINAWEZA KUBADILISHA MAISHA YA MTU
Mungu toka amemuumba mwanadamu na alimuumba mkamilifu ( ana akili timamu anaweza kufanya maamuzi ), hakuwahi kuingilia maamuzi yake
Pia pamoja na Roho Mtakatifu kukaa ndani yako lakini bado unaweza kumzimisha ( Waefeso 4:30 ) na Pia mwisho wa siku unaweza kumzimisha
1 Thesalonike 5:19 )

Maana yake pia pamoja na Roho Mtakatifu kukaa ndani yako una uhuru wa kufanya maamuzi unayotaka ( Au kutii au Kutokutii )
Mabadiliko ya Maisha yako wapi ?
Mabadiliko ya Maisha yako kwenye MAAMUZI , siku umeamua ndio siku Maisha yako yanabadilika Jumla .
AMUA KUTENDA SAWASAWA NA
ANACHOSEMA MUNGU UTAONA MAISHA YAKO YAKIBADILIKA
God bless you
Pastor Ibrahim Amasi
ABC KAHAMA
LivingWord|2020
Make a Living

Share on facebook
Share on twitter
Share on linkedin
Share on whatsapp
Share on telegram

HEKIMA ZA NDOA 5

“Ni mwanandoa mpumbavu pekee anayesubiri aombwe msamaha ili asamehe; Maana waweza kukuta kile unachoona kama kosa, mwenzako anaweza asikione hivyo, kwa kutosamehe ufa huo unaweza

Read More »

HEKIMA ZA NDOA 3

  “Kusudi la ndoa ni kujenga TIMU YA WANAOSADIANA NA KUINUANA. Wawili ni bora kuliko mmoja, MAANA MMOJA AKIANGUKA, MWENZIE ATAMUINUA. Ndoa sahihi ni muunganiko

Read More »

NDOA

“Haiunganishi familia mbili bali inazalisha familia mpya ya tatu… Inayojiendesha, kujitawala, kujiamulia na kujichagulia mambo yake… Familia hii mpya ya tatu inakuwa na kusudi na

Read More »

NDOA

Haikuanzishwa Na WANADAMU Bali MUNGU Ndiye Aliyeanzisha TAASISI HII… Imeanzishwa Na MUNGU Ambaye Ni Roho, Uwe Na Uhakika Haiwezi Kuendeshwa Kwa Kutegemea AKILI, HEKIMA NA

Read More »