“Mungu yuko kwenye program ya kuijaza mbingu kwa watu wa kila taifa, kila kabila, kila rangi, wasomi na wasio na elimu, matajiri na masikini… Jitahidi usikose mbingu maana tayari Yesu alishafia dhambi zako na kulipa gharama ya msamaha wako msalabani… Ni swala la wewe kusogea tu mahali ambapo Injili ya Kweli ya Wokovu inafundishwa na wanaoifundisha wanaiishi, kisha ukayatoa maisha yako kwa Yesu… Mbinguni kuna kadi ya mwaliko wa kuingia huko na kuishi na Yesu milele lakini unapaswa kuipokea kazi ya msalaba na kumruhusu Yesu akuokoe… Dini yako ni nzuri lakini hawana mbingu ya kukuingiza… Dhehebu lako ni zuri lakini halina mbingu ya kukupa, Yesu Kristo tu ndiye Njia pekee”
(Yohana 14:1-2,6 na Ufunuo 5:8-10).
Mwl D.C.K
MFUNGO WA SIKU 10,MASAA 12 -APRIL [SIKU YA 10]
KUISHI NJE YA UKANDA WA IBILISI (LIVING BEYOND DEVILS REACH) Ninasikia kuhusu maombi ya vita. Ni maombi maarufu ya kupigana na Ibilisi na majeshi yake.