Usipoteze Muda Kuyaweka Maneno Ya Wanadamu

 
Usipoteze Muda Kuyaweka Maneno Ya Wanadamu Kwenye Akili Yako… Wao Wakikwambia Hauwezi Kufanikiwa Au Kusogea Kwenye Maisha, Huo Ni Mtazamo Wao Na Si Wa Mungu… Hata Hivyo Mwanadamu Anajua Nini Kuhusu Yajayo? Yeye Anajua Yale Tu Anayoyaona Na Kuyasikia Ndani Ya Sekunde Aliyopo… Mwanadamu Anaweza Kukudharau Au Kukushusha Kwa Sababu Hali Yako Ya Uchumi Haiko Vizuri Leo, Lakini Hajui Kesho Unaweza Kukutana Na Vijisenti Vinazurura Ukavifuma… Wanadamu Wanafanya Makosa Makubwa Kwa Kukupangia Daraja Na Mipaka Ya Maisha Yako, Hawajui Kuwa Mungu Amekuumba Kwa Kusudi Na Mpango Maalumu… Hawajui Kuwa “You Are Loaded With Possibilities, Potentials, Talents, Gifts, Wonders etc” Wanafanya Kosa Kubwa La Kupima Kiasi Cha Mvua Kwa Kutazama Kiwango Cha Mawingu Yaliyoko Angani… Kamuulizeni Eliya na Ahabu, “WINGU KAMA NGUMI YA MTU” Lilimwaga Mvua Si Kawaida… Una Kila Kitu Ambacho Ni Rasilimali Ya Mungu Kuonesha Maajabu Yake Kupitia Wewe… Mimi Hakuna Wa Kuniambia Lolote Kuhusu Maisha Yangu, Hata Malaika Hawawezi Kuniambia Kina Cha Maisha Yangu… Najua Nimebeba Sura Na Mfano Wa Mungu, Naweza Kuumba DUNIA YANGU… Hapo Vipi? Bado Unajidharau Na Kujishusha? Unaweza Kufanya Chochote, Kila Kitu Utakacho Kupitia Kristo Akutiaye Nguvu!

Share on facebook
Share on twitter
Share on linkedin
Share on whatsapp
Share on telegram

NDOA

Haikuanzishwa Na WANADAMU Bali MUNGU Ndiye Aliyeanzisha TAASISI HII… Imeanzishwa Na MUNGU Ambaye Ni Roho, Uwe Na Uhakika Haiwezi Kuendeshwa Kwa Kutegemea AKILI, HEKIMA NA

Read More »
Mafundisho
yesunibwana

SEX BEFORE MARRIAGE

#TENDO LA NDOA KABLA YA #NDOA Luka 16:10 [10]Aliye mwaminifu katika lililo dogo sana, huwa mwaminifu katika lililo kubwa pia; na aliye dhalimu katika lililo

Read More »

KWA WAOAJI TU

“Ni Hekima Ya Mungu Kumpa Mwanadamu MALIGHAFI [Raw Materials] Ili Yeye [Mwanadamu] Afanye Sehemu Yake KUZIFANYA KUWA BIDHAA HALISI [Products]… Mungu Anakupa MTI Na Ni

Read More »